MAMBO YALIYOHARAMU KWA MWENYE JANABA,HEDHI NA NIFASI
Tumeelewa Janaba nini na hutokea katika mazingira yapi,lakin pia tumelewa Hedhi na Nifasi pamoja na mazingira yake.
Sasa ni wakati wa kujua kama mtu akiwa katika hali hizo ni mambo yapi ambayo ni haramu kwake kuyafanya.
Ikumbukwe kuwa kitu kikiwa harama humpatisha dhambi muhusika,hivyo hapa tunaposema haramu tunamaanisha kuwa mwenye JANABA,HEDHI au NIFASI hatakiwi kuyafanya na kama atayafanya basi atapata dhambi
MAMBO YALIYO HARAMU KWA MWENYE JANABA.
>Kuswali
>Kutufu{kuzunguka Al Kaaba Makka}
>Kushika Msahafu
>Kuuchukua Msahafu
>Kusoma Qur'an
MAMBO YALIYO HARAMU KWA MWENYE HEDHI AU NIFASI
>Kuswali
>Kutufu{Kuizunguka Al Kaaba Makka}
>Kushika Msahafu
>Kuuchukua au kuubeba msahafu
>Kukaa msikitini
>Kusoma Qur'an
>Kufunga
>Kupita msikitini iwapo atahofia kuuchafua msikiti
>Kuachwa
>Kumchezea kati ya kitovu na magoti

Comments
Post a Comment