Posts

Showing posts from March, 2025

ZAKATUL FITIR:MAANA YAKE,ANAEWAJIBIKA KUTOA NA NAMNA YA KUITOA

Image
  Tupo kwenye kumi la mwisho la Mwezi Mtukufu wa Ramadhani,mbali ya usiku bora kabisa wa Laylatul Qadir kupatikana kwenye kumi hili la mwisho lakini pia ndio kumi ambalo Waumini huwa wanakumbushwa watoe Zakatul Fitir ZAKATUL FITIR NI NINI? Zaka ya Fitir ni Ibada kwa Muislam kutoa kiasi cha chakula kumpa masiki kuelekea mwisho wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani,na mwisho wa kutoa Zakatul Fitir ni kabla ya kuswaliwa swala ya Iddi.Iwapo mtu atatoa baada ya swala ya Eid hiyo haitokuwa Zakatul Fitir bali Itakuwa Swadaqa kama swadaqa zingine. NANI ANAEWAJIBIKA KUTOA ZAKATUL FITIR? Kila Muislam Baleghe na mwenye akili timamu ambae kuelekea kwenye sikukuu bajeti yake ya chakula imetosheleza na imezidi hivyo kile kilichozidi anatakiwa akitoe kama Zakatul Fitir kwa kumpa Masikini. Kiongozi wa Familia atajitolea yeye na wale waliochini yake(anaowamiliki)kama Mke,watoto,mfanya kazi na  wengine lakini pia anaweza kuwatolea wazazi au ndugu wengine km akiwa na uwezo wa kufanya hivyo.Katika watoto...

NAMNA YA KUOGA KWA NIA MAALUM ILI KUTWAHARIKA.NO:1

Image
 Kuna njia mbili za kuoga nazo ni:- >Faradhi peke yake{Njia fupi} >Faradhi na sunna{Njia ndefu} Kwenye sehemu hii ya kwanza tutajifunza Faradhi za kuoga Faradhi za kuoga zipo 2 >Nia ya josho husika >Kueneza maji mwili mzima Aogae anatakiwa anuie josho analotaka kuoga km Janaba,Hedhi au Nifasi.Nia ya muogaji iende sambamba na kuanza kujimwagia maji na ahakikishe mwili wake wote unapata maji. MAANDALIZI YA KUKOGA. Tumeshatambua kuwa muogaji atanuia huku akijimwagia maji na ahakikishe mwili wote unaenea maji sasa tuangalie maandalizi ya maji na mwili kwa ujumla. Andaa ndoo safi kwa ajili ya kuogea kisha weka maji safi na hakikisha hauyatii mkono wala kidole. Andaa kata ya kuogea au kitu jingine ambacho pindi utakapokuwa unakoga maji hayatoweza kuchuruzika na kurudi kwenye ndoo ya maji. Hakikisha mwili wote hauna kitu ambacho kitazuia maji kufika kwenye ngozi km vile wigi,nywele nyingi zilizosukwa,rangi kwenye ngozi au kucha,Rami nk. Baada ya maandalizi hayo utajisaidia haj...

UJUE USIKU WA LAYLATUL QADIR

Image
LAYLATUL QADIR ni Usiku bora kabisa ambao hupatikana kwenye kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhani.Ubora wa usiku huu ALLAH Subhanahu wataalaa ameutaja  kwenye Qur'an kwa kusema" بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ   إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾ Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatil-Qadr (usiku wa Qadar).   وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾ Na nini kitakachokujulisha ni nini huo Laylatul-Qadr?   لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾ Laylatul-Qadr ni mbora kuliko miezi elfu.   تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾ Wanateremka humo Malaika na Ar-Ruwh (Jibriyl) kwa idhini ya Rabb wao kwa kila jambo. سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾ Amani mpaka kuchomoza Alfajiri.       [Al-Qadr: 1-5] Muislam anatakiwa afanye bidii kwenye kumi ili la mwisho kwa kufanya ibada za usiku ili kuweza kuupata usiku huo.Kwani mwenye kuipata Laylatul Qadir  ...

NIA YA KUOGA ILI KUONDOA JANABA,HEDHI NA NIFASI

Image
  Tumeona kuwa mwanamme anahusika na janaba tu lakini mwanamke anahusika na majosho ypute matatu,Janaba,Hedhi na Nifasi. NIA YA JANABA Nawaytu rafa'al janaba{Nanuiya kuondoa Janaba} > NIA YA HEDHI Nawaitu twaharata minal haidhwi{Nanuia kutwaharika kutokana na hedhi} >NIA YA NIFASI Nawaitu twaharata mina nifasi{Nanuia kutwaharika kutokana na nifasi}

MAMBO YALIYOHARAMU KWA MWENYE JANABA,HEDHI NA NIFASI

Image
           Tumeelewa Janaba nini na hutokea katika mazingira yapi,lakin  pia tumelewa Hedhi na Nifasi pamoja na mazingira yake. Sasa ni wakati wa kujua kama mtu akiwa katika hali hizo ni mambo yapi ambayo ni haramu kwake kuyafanya. Ikumbukwe kuwa kitu kikiwa harama humpatisha dhambi muhusika,hivyo hapa tunaposema haramu tunamaanisha kuwa mwenye JANABA,HEDHI au NIFASI   hatakiwi kuyafanya na kama atayafanya basi atapata dhambi MAMBO YALIYO HARAMU KWA MWENYE JANABA. >Kuswali >Kutufu{kuzunguka Al Kaaba Makka} >Kushika Msahafu >Kuuchukua Msahafu >Kusoma Qur'an MAMBO YALIYO HARAMU KWA MWENYE HEDHI AU NIFASI >Kuswali >Kutufu{Kuizunguka Al Kaaba Makka} >Kushika Msahafu >Kuuchukua au kuubeba msahafu >Kukaa msikitini >Kusoma Qur'an >Kufunga >Kupita msikitini iwapo atahofia kuuchafua msikiti >Kuachwa >Kumchezea kati ya kitovu na magoti

ANAEFUNGA AJIEPUSHE NA MAMBO HAYA KWANI YANAHARIBU FUNGA

Image
Umuhimu na maslahi ya Funga ya Ramadhani ni mkubwa sana.Kwani malipo na wapesi anaoupata mfungaji ndani ya Ramadhani haupatikani kwenye siku nyingine zaidi ya Ramadhani.Kutokana na hilo Mfungaji anatakiwa aichunge Funga yake ili isiharibike na kukosa fadhila na malipo makubwa ya Funga. Kwani kufunga si'KUJIZUA KULA NA KUNYWA TU'Kuna mambo mengine ambayo mfungaji anapaswa kujizuia nayo ili funga yake isiharibika. Miaongoni mwa mambo hayo ambayo mfungaji anatakiwa ayaepuke ni-: >Kusema uongo hata kama kwa utani au kwa simu >Kuteta kwa namna yoyote ile kunaharibu funga >Kufitinisha watu kunaharibu funga >Kula amini au kiapo cha uongo pia kunaharibufunga ya mfungaji >Kuangalia kwa matamanio pia kunaharibu funga ya mfungaji. Tembelea youtubechannel yetu kwa kubofya link hapo chini. https://youtu.be/5Zqyp75OLMY?si=kDkn15Zc7ZQOlDiK

TAHADHARI YA MKOJO

Image
  TAHADHARI KUHUSU MKOJO Assalaam alaykum. Naomba tukumbushane kuhusiana na najisi ya mkojo.Mkojo ni moja ya najisi ambayo baadhi yetu huichukulia ni ya kawaida sana.Haishangazi kuona mtu atakapo kuswali huenda haja ndogo mara baada ya sekunde chache kutoka msalani na kuchukua udhu kwa ajili ya swala!. TAHADHARI. Mfano wa mkojo ni kama maji yaliyo kwenye sahani ya dongo au bati.Pindi ukiyamwaga maji hayo kamwe sahani haitokuwa kavu kwa muda huo na baada ya muda kidogo utaona maji yamebaki. Hivyo hata unapoenda kujisaidia haja ndogo unatakiwa uchukue mfano huo ili nguo yako usije najisika na kuharibu swala yako.Baada ya kujisaidia chukua muda kidogo na usifanye haraka hata km unataka kuwahi swala. Kumbuka ukamilifu wa swala upo kwenye twahara. https://youtu.be/YkUVhA_Oz6c?si=H4JZaqAj2G17lqR0

IJUE TWAHARA

Image
  Twahara ni kitendo ambacho pindi kitakapokosekana haitoswihi swala. Twahara imegawanyika sehemu kuu 2.   1.Twahara kubwa   2.Twahara ndogo 1. TWAHARA KUBWA .     Hii inahusisha ukogaji kwa taratibu maalimu ikiwemo nia ya kuoga ili kuondoa hali husika na kutwaharika. Hali zinazomlazimu mtu kuoga ili kutwaharika ni 4 >J anaba >Hedhi >Nifasi >Mauti JANABA Janaba ni hali ambayo humkuta mwanamme au mwanamke. Sababu zinazopelekea mtu kuwa na janaba ni-: >Kutokwa na manii{shahawa}iwe kwa makusudi au bahati mbaya kama vile kuota,mfadhaiko.kukutana kimwili,kujichua{punyeto au kujisaga} >Kuingilia au kuingiliwa kimwili,pindi mtu atakapoingilia au kuingiliwa kimwili itakuwa amepata Janaba,Haijalishi kama atakuwa ameingilia au kuingiliwa kwa makubaliano au kulazimishwa{kubaka au kubakwa}awe amemuingilia au kuingiliwa na binaadamu au kiumbe mwingine km Jini au mnyama. >Kukutanisha tupu mbili,endapo mtu ataugusisha tupu yake kwenye tupu nyingine atakuwa...